Rais John Magufuli ameeleza mahakama kushindwa kuamua jumla ya kesi zinahusu kodi 139 kumeathiri uchumi wa nchi kwani kwa namna moja kumesababisha hata baadhi ya benki kufilisika.
Rais amesema ucheleweshwaji huo umechochea hata benki kupandisha riba kugharamia hasara zinazosababishwa na hasara itokanayo na kesi kutoamuliwa kwa wakati.
Ameongeza kuwa, ikiwa kesi hizo zingemalizika kwa wakati, serikali ingepata stahili yake lakini inashindikana. Amemtaka Jaji Mkuu, Prof Ibrahim Juma kuhakikisha kuwa kesi hizo zinafanyiwa maamuzi haraka kwa manufaa ya wananchi na uchumi wa taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |