Klabu ya Leeds United inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Uingereza, jana imemfukuza kocha wake mkuu Thomas Christiansen, baada ya matokeo ya kufungwa magoli 4-1 na Cardiff City.
Christainsen ameshindwa kupata matokeo mazuri katika mechi sita mfululizo jambo lililohatarisha nafasi ya timu hiyo katika kinyang'anyiro cha kupanda daraja msimu ujao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |