• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Russia yaitaka Marekani ifanye mazungumzo tena kuhusu ulinzi dhidi ya makombora

    (GMT+08:00) 2018-02-05 18:05:53

    Naibu waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergey Ryabkov amesema Russia na Marekani zinapaswa kurudia mazungumzo kuhusu ulinzi dhidi ya makombora.

    Akizungumza na gazeti la Izvestia nchini Russia, Bw. Ryabkov alikumbusha kuwa uhusiano wa karibu kati ya silaha za maangamizi za kimkakati na ulinzi dhidi ya makombora umeandikwa katika dibaji ya Makakati wa Kupunguza Silaha za Maangamizi (START) .

    Ameongeza kuwa kwa muda mrefu hakuna mazungumzo maalum na thabiti yaliyofanyika kuhusu suala hilo kati ya Russia na Marekani. Sasa wakati umefika yanapaswa kufanyika tena.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako