Mjumbe wa taifa wa China Bw. Yang Jiechi atafanya ziara ya siku mbili nchini Marekani kuanzia alhamis wiki hii. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bw. Geng Shuang amesema, hivi karibuni, nchi hizo mbili zimeeleza matumaini ya kuendelea kudumisha na kuzidisha mawasiliano katika sekta mbalimbali. Katika ziara hiyo, Bw. Yang atabadilishana maoni na maofisa wa Marekani kuhusu uhusiano kati ya China na Marekani na masuala ya kimataifa na kikanda yanayofuatiliwa kwa pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |