Chama cha soka nchini Uholanzi KNVB leo jumanne kinatarajia kumtangaza Ronald Koeman kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa.
Koeman ambaye alitimuliwa kazi na klabu ya Everton mwezi Oktoba mwaka jana, anatarajia kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Dick Advocaat aliyejiuzulu baada ya timu hiyo kukosa nafasi ya kuzu kombe la dunia.
Kazi kubwa ya Koeman kwa mujibu wa Chama hicho, itakuwa ni kurejesha tumaini la mashabiki wa taifa hilo lenye historia nzuri ya soka, na kuliongoza katika maandalizi ya kufuzu fainali za Ulaya mwaka 2020 pamoja na kombe la dunia mwaka 2022.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |