• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Wafanyakazi wa mifuko ya jamii Tanzania kulindwa

    (GMT+08:00) 2018-02-06 18:45:07
    Serikali ya Tanzania imewahakikishia waliokuwa wafanyakazi wa mifuko ya umma ya hifadhi ya jamii iliyounganishwa na kuunda Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kuwa, hakuna atakayepoteza ajira yake kutokana na kuunganishwa kwa mifuko hiyo.

    Imesema kuunganisha mifuko hiyo, hakumaanishi kuwa waliokuwa wafanyakazi katika mifuko hiyo watapoteza ajira zao. Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii imepitishwa bungeni na hivyo inasubiri saini ya Rais kuwa sheria na kuanza kutumika wakati huo, Serikali ikishughulikia kanuni ikiwemo ya kuweka kikokotoleo cha kiwango cha mafao ya kuliwapa wastaafu.

    Akijibu hoja zilizotolewa na wabunge mbalimbali wakati wakichangia Muswada wa kuundwa kwa sheria hiyo bungeni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira, Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama alisema wafanyakazi hao wasiwe na wasiwasi kwani ajira zao zipo salama. Hata hivyo alisema, watakaoondolewa ni wasio waadilifu na wasioendana na utendaji wa mfuko.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako