• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda:Shule 22 za kibinafsi zapokonywa leseni

    (GMT+08:00) 2018-02-09 17:38:42

    Takriban shule 22 za kibinafsi zimepokonywa leseni za kuendesha biashara zao jijini Kampala baada ya kukosa vigezo vinavyohitajika na wizara ya elimu.

    Halmashauri ya masuala ya elimu ya Uganda imechukua uamuzi huo baada ya kutoa ilani kwa sule 48 kurekebisha viwango vyao mwezi wa January.

    Shule hizo zinazodaiwa kuzingatia biashara zaidi ya viwango na mazingira ya elimu zimefungwa baada ya kukosa ua la wanafunzi kuendesha shughuli zao,kukosa vyoo,waalimu waliohitimu na vifaa vya masomo.

    Ambrose Atwoko mkurugenzi wa halmashauri hiyo amesema uamuzi huo unatakiwa kuungwa mkono na wazazi kwa ajili ya maendeleo ya elimu bora kwa wanafunzi .

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako