Wizara ya serikali za mitaa ya Libya imesema Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa mataifa UNDP limetoa dola za kimarekani milioni 17 kufadhili miradi midogo katika baadhi ya miji nchini Libya. Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo inasema, fedha hizo zitatumiwa kusaidia baadhi ya makampuni madogomadogo nchini humo, lakini haikutaja ni miradi gani inayolengwa kwenye mpango huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |