• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Makamu wa rais wa Tanzania azindua mradi wa Benki ya Dunia kutangaza utalii nchini humo

    (GMT+08:00) 2018-02-13 08:57:57

    Makamu wa rais wa Tanzania Bi. Samia Suluhu Hassan jana amezindua mradi uliofadhiliwa na Benki ya Dunia unaolenga kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko nchini humo.

    Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika eneo la Kihesa-Kilolo, Bi. Samia ameishukuru Benki ya Dunia kwa kuunga mkono sekta ya utalii nchini Tanzania, na kusema mradi huo una maana kubwa kwani utasaidia kuwaondoa watu katika umasikini uliokithiri. Ameuelezea mradi huo, Usimamizi wa Maliasili kwa Utalii na Ukuaji (REGROW), kuwa nyenzo mpya katika kutangaza utalii katika eneo la kusini mwa Tanzania ambalo lina vivutio vingi vya utalii lakini havifahamiki sana.

    Mradi wa REGROW umeanzishwa ili kukabiliana na changamoto za kuboresha miundombinu ikiwemo barabara, kuweza kufikia vivutio hivyo vya utalii.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako