• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya kuvutia kampuni nyingi za ndege ili kuendeleza sekta ya utalii

    (GMT+08:00) 2018-02-13 09:11:50

    Waziri wa Utalii wa Kenya Bw. Najib Balala amesema nchi hiyo inatafuta kuzivutia kampuni zaidi za ndege kuzindua safari kwenda nchini humo ili kuendeleza sekta ya utalii.

    Akizungumza kwenye kongamano la utalii jijini Nairobi, Bw. Balala amesema sekta ya utalii haifanyi vizuri kutokana na uwezo mdogo wa usafiri wa anga nchini humo. Amesema karibu kampuni kumi za ndege zinafanya safari nchini Kenya, na kwamba lengo ni kuongeza idadi hiyo hadi zaidi ya 20 ili kupata watalii wengi zaidi.

    Takwimu zilizotolewa na serikali zinaonyesha kuwa karibu wageni milioni 1.47 wa kimataifa wamefanya utalii nchini Kenya mwaka 2017, wakati lengo ni wageni milioni tatu.

    Aidha amesema sekta ya utalii nchini humo inapaswa kufanya mageuzi kuendana na mwelekeo wa kimataifa ili kuongeza mchango wake kwa uchumi wa Kenya na kuunda fursa nyingi za ajira.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako