Wakulima wa maua nchini Kenya wamelalamikia huduma ya umeme isiyo na uhakika katika eneo la Naivasha na kusema tatizo hilo linaathiri uzalishaji.
Wakiongea kuelekea siku ya Wapendanao inayosherehekewa Jumatano, wakulima hao wamesema kuongezeka kwa gharama za uzalishaji na wafanyakazi ni changamoto kubwa inayoikabili sekta hiyo hivi sasa.
Kwa mujibu wa Meneja wa Rasilimali Watu wa Kampuni ya Mawardi ya Van-Deng-Berg, George Onyango, awali walikuwa wakisafirisha mashina laki 5 ya mawardi kila siku nchini Ujerumani na Holand. Hata hivyo, Onyango anasema bei ya shina moja la waridi imesalia palepale kwa miaka mingi ikilinganishwa na kupanda kwa gharama za pembejeo za kampuni na usafirishaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |