Wakulima wa maua nchini Kenya wamelalamikia kuendelea kupanda kwa bei ya uzalishaji ambayo imepunguza faida yao kwenye sekta hiyo inayoajiri mamia ya watu.
Wamesema hali imeathiriwa zaidi na kukatika kwa mara kwa mara kwa umeme hali inayowalazimu kutumia jenereta na hivyo kutumia fedha zaidi kununua mafuta.
Wadau kwenye sekta ya maua wanatarajia mauzo ya juu kati ya leo na kesho wakati wa maadhimisho ya sikukuu ya wapendanao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |