• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakimbizi kutoka DRC wafariki katika Ziwa Albert wakikimbilia nchini Uganda

    (GMT+08:00) 2018-02-14 08:00:09

    Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema, wakimbizi wanne kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wamekufa maji baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuelekea nchini Uganda kuzama katika Ziwa Albert.

    Msemaji wa UNHCR Babar Baloch amesema, wiki iliyopita zaidi ya wakimbizi 22,000 toka DRC walivuka Ziwa Albert kuelekea Uganda, na kufanya idadi ya jumla ya wakimbizi 34,000 kuingia nchini Uganda tangu mwaka huu uanze.

    Kutokana na mapigano yanayoendelea katika jimbo la Ituri nchini DRC, idadi kubwa ya wakimbizi hukimbia makazi yao na kuingia nchi za Uganda na Tanzania kupitia Ziwa Albert.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako