Mchezaji wa klabu ya Hull City nchini Uingereza Ryan Mason amelazimika kustaafu akiwa na umri wa miaka 26 kutokana jeraha la fuvu la kichwa alilopata katika mechi dhidi ya Chelsea mwaka 2017.
Mason ambaye aliichezea timu ya taifa ya Uingereza mara moja mwaka 2015 alilazimika kufanyiwa upasuaji baada ya kugongana vichwa na beki wa Chelsea Gary Cahill.
Uamuzi wake wa kustaafu unafuatia ushauri wa madaktari wa upasuaji wa neva.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |