• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Ufaransa atishia kuishambulia Syria

    (GMT+08:00) 2018-02-16 16:44:45
    Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametishia kuishambulia Syria ikiwa ushahidi utaibuka kuwa serikali ya Syria inatumia silaha za kemikali dhidi ya raia.

    Lakini Bw Macron alisema kuwa uchunguzi bado haujaonyesha kuwa silaha zilizoharamishwa zimetumiwa.

    Matamshi yake yanafuatia ripoti kadhaa za mashambulizi ya kutumia silaha za Chlorine nchini Syria tangu mwezi Januari.

    Watu tisa walitibiwa kwa matatizo ya kupumua baada ya bomu linaloaminwa kujazwa na kemikali kuangushwa katika mji unaoshikiliwa na waasi mapema mwezi huu.

    Upinzani nchini Syria ulisema kuwa helikopta ya serikali iliangusha bomu eneo la Saraqeb katika mkoa ulio kaskazini mashariki wa Idlib.

    Serikali ya Syria inakana kutumia silaha za kemikali na kusema kuwa haiwalengi raia.

    Akiongea mjini Paris siku ya Jumanne Macron alielezea msimamo wake kuwa matumizi ya silaha za kemikali ni kuvuka mstari mwekundu wa serikali yake.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako