Timu ya Yanga ya Dar es salaam, imefanikiwa kwenda raundi ya kwanza ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika licha ya sare ya bao 1-1 na wenyeji wao Saint Louis Suns United katika mchezo wa marudiano wa raundi ya awali kipute kilichopigwa uwanja wa Linite mjini Victoria Shelisheli. Yanga sasa itakutana na Township Rollers ya Botswana iliyofanikiwa kuichabanga El Merreikh ya Sudan.
Gor Mahia ya Kenya nayo imefanikiwa kufuzu raundi ya kwanza ya michuano hiyo baada ya kuifunga