Mkurugenzi mkuu wa idara ya uhusiano na ushirikiano wa kimataifa ya Afrika Kusini anayeshughulikia mambo ya Asia ya mashariki na Oceania Bw. Manelisi Genge amesema kuwa China ni mwenzi muhimu wa Afrika Kusini na uhusiano kati ya nchi hizo mbili umefikia kiwango kipya cha juu.
Bw. Genge ameyasema hayo kwenye shughuli ya kuadhimisha miaka 20 tangu China na Afrika Kusini kuanzisha uhusiano wa kibalozi.
Ameongeza kuwa, nchi yake itaendelea kupiga hatua katika uhusiano na China katika Nyanja za kisiasa, uchumi na utamaduni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |