• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Marais wa Tanzania na Kenya waingilia kati kutatua migogoro ya kibiashara baina ya nchi hizo zao

    (GMT+08:00) 2018-02-23 20:53:59

    Rais wa Tanzania John Magufuli na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta wamewaagiza mawaziri wao kutatua migogoro inayokwamisha shughuli za kibiashara baina ya mataifa hayo ya Afrika Mashariki.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kurugenzi ya mawasiliano ya Rais Ikulu ya Dar es Salaam, viongozi hao wametoa maagizo hayo walipokutana mjini Kampala nchini Uganda muda mfupi kabla ya kuanza mkutano wa viongozi wa mataifa ya Afrika Mashariki.

    Taarifa hiyo inaeleza kuwa marais hao wana nia ya kuendelea kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa hayo jirani, na taarifa hiyo pia ikieleza kuwa viongozi hao wamesikitishwa baada ya kujua kuwa migogoro hiyo imetokana na sababu ndogo kabisa.

    Mapema mwezi huu, nchi hizo zimekubaliana kumaliza migongano ya kibiashara, na kufungua njia kwa ajili ya kuendeleza biashara baina ya mataifa ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

    Takwimu zinaonyesha kuwa Kenya na Tanzania zinafanya asilimia 45 ya biashara nzima ya jumuiya ya Afrika Mashariki.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako