Rais Uhuru Kenyatta ameagiza kuanzishwa kwa mchezo wa gofu katika shule za umma kote nchini Kenya, kwa lengo la kuukuza na kufikia viwango vya kimataifa.
Uhuru Kenyatta ameyasema hayo wakati anakabidhi bendera ya taifa kwa timu ya taifa ya vijana inayokwenda kushiriki mashindano ya vijana nchini Morocco yanayoanza Machi 3 na kumalizika machi 10 mjini Cassablanca.
Kenya ni miongoni mwa mataifa 18 yanayoshiriki mashindano hayo ya Afrika kwa vijana yajulikanayo kama All Africa Junior Golf Championship.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |