Benki ya Co-operative nchini Kenya itapokea mkopo wa dola milioni 150 kutoka kwa shirika la fedha la kimataifa IFC.
Mkopo huo ambao Co-operative italipa ndani ya miaka 7 inatarajia kukopesha makapuni na mashiririka madogo madogo.
IFC imesema kwenye taarifa kwamba mkopo huo utawezesha Co-operative kuongeza uwezo wake wa kutoa huduma za kifedha za muda mrefu hasa kwa biashara za wastani na zile ndogo ndogo.
Co-operative ina matawi 149 kote nchini Kenya na wateja wapatao milioni 6.5.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |