Usimamizi wa maduka ya jumla ya Nakumatt utaendelea tena hatua ya kupunguza wafanyikazi wake ili kukabiliana na changamoto za fedha.
Peter Kahi mratibu wa maduka hayo amesema wanajizatiti kuhakikisha wanaendelea na biashara hiyo pamoja na kupunguza gharama na madeni.
Biashara hiyo ya familia imeagizwa kusimamiwa na waratibu ili kuregesha madeni ya wadau baada ya kutangazwa na mahakama kuu kufilisika.
Muungano wa wafanyikazi hata hivyo umeagiza wahudumu hao kulipwa fidia ya shilingi laki 2.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |