Raia wengi wa Rwanda wanaendelea kutumia gesi kupikia badala ya Makaa.
Taakwimu kutoka kwa uagiziaji wa gesi zinaonyesha kuwa ununuaji nje wa bidhaa hiyo umeongezeka mara 14 ndani ya miaka 17.
Mwaka wa 2010 Rwanda iliagizia zaidi ya kilo 700,000 za gesi lakini hadi kufikia mwaka 2017 ilikuwa imeagizia kilo milioni 10.
Serikali ya Rwanda imekuwa ikiwahimiza raia kutumia kawi safi kwa shughuli za upishi ili kupunguza ukataji miti na hivyo kulinda mazingira.
Kulingana na shirika la afya duniani WHO zaidi ya watu milioni 4 hufariki kila mwaka kutokana na maradhi yanayotokana na uchafuzi wa hewa nyumbani kaa vile kutumia kuni, makaa na mafuta ya taa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |