• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa China akutana na mjumbe maalumu wa rais wa Korea Kusini

    (GMT+08:00) 2018-03-12 20:48:25

    Rais Xi Jinping wa China leo hapa Beijing amekutana na mjumbe maalumu wa rais wa Korea Kusini ambaye pia ni mshauri mkuu wa usalama wa kitaifa , Bw. Chung Eui-yong.

    Rais Xi amesema, China inafurahia mjumbe maalumu wa rais wa Korea Kusini kuja hapa China kufahamisha kuhusu hali ya ziara yake nchini Korea Kaskazini, na kwenda Marekani kuhimiza mazungumzo kati ya Korea Kaskazini na Marekani. Amesema China siku zote inaunga mkono pande mbili za Peninsula ya Korea kuboresha uhusiano, kuhimiza ushirkiano na maafikiano, kuunga mkono Marekani na Korea Kaskazini kufanya mazungumzo na kutatua ufuatiliaji wa pande mbili kwa mazungumzo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako