Mahakama Kuu imesimamisha Mamlaka ya Mapato ya Kenya kutoza ushuru kwenye maji ya chupa, vinywaji visivyo na pombe na vipodozi.
Jaji John Mativo amesema utozwaji wa ushuru kwenye bidhaa hizo haindani na sheria.
Aidha amesema kutozwa kwa ushuru hujenga mzigo wa kodi kwa umma na wazalishaji.
Jaji Mativo alielezea kuwa kodi inapaswa kuwekwa tu kulingana na maadili ya kitaifa na kanuni za utawala kati yao usawa na haki katika uwekaji wa kodi.
Hatua hii, inaangalia kulinda umma kutokana na gharama za juu za maisha zinazoletwa na ushuru.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |