Timu ya Riadha kutoka Kenya imewasili nchini Algeria kwa ajili ya mashindano ya tano ya mbio za nyika ya barani Afrika yanayotarajiwa kufanyika siku ya jumamosi.
Kikosi hicho kunajumisha wanamichezo 30, wakiwemo viongozi wa timu, makocha pamoja na wanariadha.
Kwa upande wa wanariadha, timu hiyo imegawanywa mara nne, wakubwa mbili (wanawake kwa wanaume) na vijana (wanawake kwa wanaume), na kila timu inawanariadha sita.
Katika msimu uliopita wa mashindano kama hayo nchini Cameroun, Kenya ilishinda medali Nane za Dhahabu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |