CHAMA Cha Riadha Zanzibar (ZAAA) kimefuta uvumi kuwa kimekataa kufanya uchaguzi wa viongozi, kwa kujieleza kuwa, kinayo nia ya kufanya hivyo lakini kikwazo kikubwa kilichopo ni kutopata uwezeshaji kutoka Baraza la Taifa la Michezo Zanzibar (BTMZ).
Katibu wa chama hicho amefafanua suala kilo kuwa, wao kama viongozi walishatoa taarifa mapema kwa BMTZ, na wanasubiri majibu ambayo yatatoa tarehe rasmi ya uchaguzi.
Kuhusu viongozi walioko madarakani kumaliza muda wao, katibu huyo amesema kwa muujibu wa katiba ya chama, ni kweli muda wao uliisha tangu Disemba mwaka jana na wanasubiri tarehe ya uchaguzi kutoka BMTZ.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |