Droo kwa ajili ya kupanga mechi za robo fainali za klabu bingwa Ulaya inatarajiwa kufanyika kesho ijumaa katika makao makuu ya UEFA mjini Nyon nchini Uswisi majira ya saa nane mchana kwa saa za Afrika Mashariki.
Timu nane zitakazopambanishwa katika droo hiyo ni Barcelona (Hispania), Bayern München (Ujerumani), Juventus (Italia), Liverpool (Uingereza), Manchester City (Uingereza)
Real Madrid (Hispania), Roma (Italia) na Sevilla (Hispania).
Mechi za robo fainali zinatarajiwa kupigwa tarehe 3 na 4 mwezi Aprili, ikiwa ni mechi za awali, na marudiano tarehe 10 na 11 mwezi Aprili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |