• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania:Magufuli afungua miradi ya maendeleo

    (GMT+08:00) 2018-03-15 20:51:26

    RAIS John Magufuli ametangaza fursa nane kabambe ambazo serikali yake ya awamu ya tano imepanga kuwaletea wananchi wanyonge wa Tanzania, ikiwemo ajira.

    Katika suala hilo la ajira, Rais Magufuli amesema serikali yake imejibu suala la uhaba wa ajira nchini kwa vitendo kwa kutengeneza ajira takribani milioni moja kutokana na kuanzisha miradi mbalimbali nchini. Kati ya miradi hiyo, Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) pekee umezalisha ajira takribani 30,000 za moja kwa moja na ajira zaidi ya 600,000 zinazohusu watu mbalimbali watakaojiajiri kwa kutoa huduma kwa wafanyakazi katika mradi huo.

    Rais Magufuli alitambia mafanikio iliyopata serikali ya awamu ya tano katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wake wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa reli hiyo ya kisasa katika eneo la Ihumwa, umbali wa kilometa 15 kutoka Mjini Dodoma. Alitaja mifano ya miradi mingine inayozalisha ajira kuwa ni pamoja na mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, zaidi ya ajira 15,000, mradi wa Umeme Rufiji ajira 20,000, barabara mijini ajira 30,000, barabara vijijini ajira 70,000 na miradi ya umeme vijijini, ujenzi wa meli na miundombinu mingine inayozalisha mamilioni ya ajira.

    Rais Magufuli alisema, utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa reli kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza, baadaye Kigoma, Rwanda na Burundi, unatakiwa kusimamiwa kwa karibu na wizara hivyo akatoa mwito kwa wizara, mhandisi mshauri na mkandarasi mjenzi kuhakikisha unamalizika kwa wakati. Ukombozi kwa watumishi waliohamishiwa Dodoma Alisema kutokana na reli hiyo Tanzania na hasa Dodoma itakuwa kama Ulaya ambako mtu anaishi Dar es Salaam na anafanya kazi Dodoma, kwani atahitaji saa tatu tu kusafiri kutokana na kasi ya kilometa 160 kwa saa katika umbali wa kilometa 522.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako