• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Wales Ryan Giggs amemtema Aaron Ramsey

    (GMT+08:00) 2018-03-16 09:04:56

    Mchezaji wa zamani wa Man United Ryan Giggs ambaye kwa sasa ni kocha mkuu wa timu ya taifa ya Wales amemtema Aaron Ramsey kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Wales kinachojiandaa na kombe la China.

    Giggs ametangaza kikosi hicho mapema jana na kumjumuisha mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid Gareth Bale ambaye msimu huu sio mzuri sana kwake kutokana na majeraha ya mara kwa mara.

    Pia wameingizwa wachezaji wapya katika kikosi hicho wakiwemo beki wa Brentford Chris Memphan, Beki wa Swansea Connor Roberts, kiungo wa Preston Billy Bodin, na golikipa wa Ipswich Michael Crowe.

    Beki kisiki wa Everton Ashley William ataendelea kuwa nahodha wa timu hiyo. Mshambuliaji hatari wa West Bromwich Robson Kanu hayupo katika kikosi hicho huku David Brook nae akitoswa kutokana na kuugua.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako