Wasangaji tayari washanza kuagiza mifuko milioni 6.6 ya mahindi kutoka Uganda, huku wakulima katika bonde la ufa wanalia kutengwa na mavuno yao baada ya wizara ya kilimo kupunguza chini ununuzi.
Wakulima sasa wanasema kuwa biashara ya mpakani ya nafaka inawaumiza wakati wasagaji wanafaidika.
Aidha wameiomba serikali kuzuia uagizaji wa nafaka, wakisema wasagaji wanatumia fursa ya soko la pamoja la Afrika Mashariki kuagiza mahindi kutoka Uganda na kuweka akiba ya mazao ili kusababisha uhaba/ ukosefu wa bandia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |