• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tantrade waongeza thamani mazao ya kilimo

    (GMT+08:00) 2018-03-19 19:33:38
    MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), imesema imeanza kuongeza thamani ya mazao ya kilimo visiwani Zanzibar kwa kushirikiana na sekta ya utalii.

    Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tantrade, Edwin Rutageruka alisema hayo aliposhiriki katika mjadala wa Jukwaa la Fursa za biashara Zanzibar.

    Aidha alisema mwishoni mwa mwaka huu, wanatarajia kwenda nchini Afrika Kusini na Kenya katika biashara na uwekezaji wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Muungano.

    Amesema kwa sasa (TanTrade), wanaweka mkakati katika kuongeza thamani ya mazao kama mwani ambao unaweza kuzalisha zaidi ya bidhaa 46 na kuacha kusafirisha zikiwa hazina thamani na kuuzwa kwa Sh 500 kwa kilo.

    Rutageruka alisema wanatarajia kuanzisha viwanda vya kuzalisha bidhaa hizo ikiwemo sabuni na kwamba watahakikisha watalii wanaoingia visiwani humo wanatumia bidhaa na kusaidia kutoa ajira na kukuza uchumi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako