Umoja wa Ulaya na Marekani zimeliambia Shirika la biashara duniani WTO, kuwa serikali ya Marekani imekataa mapendekezo yaliyotolewa na Umoja wa Ulaya juu ya ushuru uliotozwa na Marekani kwa bidhaa za nishati ya jua. Taarifa iliyotolewa jana na WTO inasema pande hizo mbili hazikufikia makubaliano, lakini zitasimamia athari ya ushuru huo kwa biashara na kuendelea na mazungumzo. Mwezi Januari, serikali ya Marekani ilitangaza kutoza ushuru wa asilimia 50 kwa mashine za kufulia nguo na ushuru wa asilimia 30 kwa bidhaa za nishati ya jua zinazoingizwa nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |