Manchester United imeongeza mkataba wa mwaka mmoja na mchezaji wake Ashley Young ambao utamfanya asalie hapo hadi mwaka 2019.
Mkataba wa awali wa Young unamalizika mwishoni mwa msimu huu, lakini kutokana na maoni ya kocha Jose Mourinho aliyedai kuridhishwa na kiwango cha nyota huyo, umeongezwa.
Young alijiunga na United akitokea Aston Villa mwaka 2011.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |