Watu 26 wameuawa na wengine 18 kujeruhiwa baada ya mtu mmoja kujilipua kwa bomu karibu na Chuo Kikuu cha Kabul nchini Afghanistan mapema leo.
Ofisa mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake amesema, huenda mtu huyo alitaka kujilipua kwenye Hekalu la Sakhi ambako maelfu ya watu walikusanyika kusherehekea mwaka mpya wa nchi hiyo, ila kutokana na ulinzi mkali alishindwa kufika eneo hilo hivyo kujilipua karibu na Chuo Kikuu hicho.
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Afghanistan haijatoa tamko lolote kuhusiana na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |