Wizara ya mambo ya nje ya Russia imesema inatumai kuwa Uingereza itaweka wazi nyaraka zote kuhusu tukio la kuwekewa sumu kwa aliyekuwa jasusi wa Russia Bw. Sergei Scripal na binti yake Yulia nchini Uingereza, na kusema iko tayari kushirikiana na Uingereza kwenye uchunguzi wa tukio hilo. Wizara hiyo imesisitiza kuwa Russia haihusiki na tukio hilo kwa kuwa kufanya hivyo hakuna manufaa yoyote kwa Russia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |