Timu ya riadha ya Kenya wanwake imepata pigo kwenye mashindano ya dunia ya nusu marathon yanayoanza jumamosi ijayo mjini Valencia nchini Hispania baada ya nyota wake wawili kujiondoa katika dakika za mwisho.
Wanariadha waliojiondoa ni Mshindi wa tatu katika mbio hizo za mwaka 2016 Mary Wacera, na bingwa wa marathoni fupi Fancy Chemutai.
Kutokana na hilo, timu hiyo sasa italazimika kuwakilishwa na wanariadha watatu waliosalia baada ya juhudi za kuweka mbadala wao kugongwa mwamba kufuatia muda wa usajili kufungwa rasmi siku ya jumatatu iliyopita.
Lakini kwa upande wa wanaume timu hiyo imekamilika kwa kuwa na wanariadha wote watano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |