• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Droo ya kombe la CAF: Klabu kutoka Afrika Mashariki zawajua wapinzani wake

    (GMT+08:00) 2018-03-22 09:54:52

    Gor Mahia (Kenya), Young Africans (Tanzania) na Rayon Sport (Rwanda) zimefahamu wapinzani wake katika mechi za mtoano zitakazoamua timu za kushiriki hatua ya makundi ya kombe kwa shirikisho la vilabu barani Afrika.

    Katika droo iliyochezeshwa jana mjini Cairo, Young Africans imepangwa kucheza na Wolaita Dicha ya Ethiopia, Rayon Sport itacheza dhidi ya Costa do Sol ya Msumbiji na Gor Mahia dhidi ya Supersport United ya Afrika Kusini.

    Kwenye mechi za kwanza za hatua hiyo, timu zote tatu zitakuwa nyumbani kati ya Aprili 6-8 na kwenda ugenini Aprili 17-18 na endapo zitafuzu basi moja kwa moja zitaingia kwenye droo ya hatua ya makundi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako