Waziri wa habari na utamaduni wa Nigeria Bw. Lai Mohammed amesema mvulana mmoja na wasichana 105 waliotekwa na kundi la Boko Haram wameachiwa huru bila masharti na bila kutoa malipo yoyote, na hakuna mpiganaji wa kundi la Boko Haram aliyebadilishwa na wanafunzi hao.
Bw. Mohammed amethibitisha kwamba watu hao wamekabidhiwa kwa serikali ya Nigeria.
Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema Bw. Antonio Guterres amekaribisha kuachiwa kwa wasichana hao wakiwa salama, na kuhimiza serikali kuwafikisha wale waliohusika na tendo hilo mbele ya sheria haraka iwezekanavyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |