Serikali ya Ethiopia imekataa ripoti kuwa hali ya dharura ya miezi sita iliyowekwa hivi karibuni imeathiri vibaya sekta ya utalii.
Hapo awali serikali ya Ethiopia imeeleza kuwa hali ya dharura ya miezi 10 ilileta changamoto katika juhudi za kuvutia watalii wa kigeni, na wachambuzi wanasisitiza kuwa hali ya dharura ya sasa pia inaleta changamoto kama hizo katika sekta hiyo.
Mkurugenzi wa Wizara ya umma na uhusiano wa kimataifa Bw. Gezahegn Abate, amebainisha kwamba amani na utulivu ni muhimu kwa sekta ya utalii, na hali ya dharura itaisaidia Ethiopia kufanikisha lengo la kuleta amani na utulivu nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |