Wizara ya mambo ya nje ya Marekani na serikali ya Jordan wamezindua taasisi mpya ya kikanda ya kutoa mafunzo ya kupambana na ugaidi kusini mwa mji wa Amman. Mwana mfalme wa Jordan Rashid na msaidizi wa waziri wa mambo ya nje wa Marekani anayeshughukia usalama wa kidiplomasia Bw. Michael Evanoff, walizindua rasmi taasisi hiyo iliyofadhiliwa, kujengwa na kupatiwa vifaa kupitia mpango wa misaada ya kupambana na ugaidi ATA wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |