Mkutano wa majira ya spring wa viongozi wa Umoja wa Ulaya umeanza jana huko Brussles, Ubelgiji.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Mwenyekiti wa baraza la Ulaya Bw. Donald Tusk amesema inahitaji kuzuia vitendo vya kujilinda kibiashara duniani kote, na kufanya mazungumzo na Marekani ni muhimu zaidi.
Katika mkutano huo, viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya walijadiliana na Gavana wa Benki Kuu ya Ulaya Bw. Mario Draghi kuhusu hali ya uchumi ya sasa. Bw. Tusk amesema, hivi sasa hali ya uchumi inaendelea vizuri lakini haimaanishi kuwa masuala yote yanaweza kutatuliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |