Rais Recep Erdogan wa Uturuki ametangaza kuanza kwa operesheni za kijeshi kwenye eneo la Sinjar nchini Iraq, baada ya kupata ushindi kwenye operesheni mjini Afrin. Akiongea kwenye mkutano wa chama chake uliofanyika katika mkoa wa Trabzon, rais Erdogan amesema vikosi vya Uturuki vitatwaa udhibiti wa mji wa Tel Rifaat ulioko kaskazini mwa Syria unaodhibitiwa na wapiganaji wakurdi. Pia rais huyo ameihimiza Marekani kukabidhi udhibiti wa eneo la Manbij la Syria kutoka kundi la YPG kwa "wamiliki wa kweli wa mji huo", la sivyo jeshi la Uturuki litawaondoa kutoka mjini humo kwa msaada kutoka kwa watu wa Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |