Sebastian Vettel wa Ujerumani ameshinda taji la mbio za kwanza za mashindano ya magari ya mwendokasi maarufu kama Langalanga, zilizofanyika jana mjini Melbourne nchini Australia.
Katika mzunguko wa mwisho katika sakiti hiyo yenye urefu wa kilomita 5.4 alifanikiwa kuwapita madereva wawili waliokuwa mbele yake, Lewis Hamilton wa timu ya Mercedes aliyeshika nafasi ya pili na dereva mwenzake wa timu ya Ferrari Kimi Raikkonnen aliyeshika nafasi ya tatu.
Kwa ushindi huu Vettel amefanikiwa kutetea taji hilo ambalo hata msimu uliopita alifanikiwa kulitwaa.
Kukamilika kwa mbio hizi za kwanza kunawapa madereva muda wa kujiandaa na mbio za Bahrain zitakazofanyika April 8 mjini Sakhir.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |