Taarifa iliyotolewa na idara ya mambo ya dharura ya Russia inasema watu 64 wamethibitishwa kufariki dunia kutokana na ajali ya moto iliyotokea jumapili alasiri kwenye jumba moja la maduka mjini Kemerovo. Hivi sasa idara husika zinaendelea na uchunguzi ili kuthibitisha chanzo cha ajali hiyo, na majumba yote ya maduka kama hilo kote nchini Russia yanafanyiwa ukaguzi, ili kuzuia ajali kama hiyo isitokee tena.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |