Idara ya usalama ya mkoa wa mpakani wa Krasnoyarsk nchini Russia imewakamata watu tisa wanaohusika na shughuli za kigaidi. Kwa mujibu wa idara hiyo, watu hao wamethibitishwa kuwa na uhusiano na makundi ya kigaidi ya kimataifa, baadhi yao wamekiri kujihusisha na shughuli za kigaidi, na watakabiliwa na mashtaka ya makosa ya jinai. Hivi sasa uchunguzi unaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |