Mchezaji wa klabu ya Real Madrid Francisco Suarez (Isco) amefunga magoli matatu (hat-trick) na kuchangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa timu yake ya taifa wa 6-1 iliopata dhidi ya wababe wa soka kutoka Amerika ya Kusini Argentina.
Goli la kufutia machozi la Argentina iliyocheza bila Messi ambaye ni majeruhi lilifungwa na Nicolas Otamendi katika dakika ya 39.
Hii ni mechi ya 18 mfululizo kwa Hispania kucheza bila kufungwa tangu waondolewe kwenye hatua ya michuano ya Ulaya mwaka 2016.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |