Ikulu ya Russia imesema Rais Vladimir Putin ameamuru ukaguzi wa kiusalama ufanywe kila baada ya muda kwenye majumba makubwa ya maduka baada ya ajali kubwa ya moto kutokea mjini Kemerovo. Rais Putin ameiagiza serikali kuu na serikali za majimbo kutoa msaada wa lazima kwa familia za wahanga wa ajali hiyo iliyosababisha vifo vya watu 64, pia amesisitiza kuwa uchunguzi unatakiwa kufanyika kwa uwazi, ili kuthibitisha chanzo cha ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |