Kamishna mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi wa Palestina Bw. Pierre Krahenbuhl ameonya dhidi ya kudorora kwa hali ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza.
Akiongea na wanahabari katika mji wa Khan Younis, Bw. Krahenbuhl amesema hakuna mtu yeyote anayeweza kupunguza hali katika sehemu ya Gaza, ambayo inatawaliwa na kundi la Hamas.
Amesema shirika lake linafuatilia matokeo mabaya ya kibinadamu katika ukanda wa Gaza kutokana na kuongezeka kwa kiasi kikubwa kwa kiwango cha ukosefu wa ajira na kushindwa kwa familia kukidhi mahitaji ya maisha ya kawaida.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |