• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kiongozi wa AU ataja hatua za upande mmoja tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia

    (GMT+08:00) 2018-03-29 09:32:15

    Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bw. Moussa Faki Mahamat amesema hatua za upande mmoja zinaweza kuwa ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa dunia.

    Akiongea kwenye mjadala wa njia ya simu wa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hatua za pamoja za kuimarisha operesheni za kulinda amani za Umoja wa Mataifa, Bw. Mahamat amesema kila juhudi zinapaswa kufanywa kulinda utaratibu wa pande nyingi.

    Amesema operesheni za kulinda amani zilizoidhinishwa na Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, ni msingi wa juhudi za kimataifa za kuhimiza amani na usalama, ambazo zinaonesha umuhimu wa utaratibu wa pande nyingi na mshikamano wa dunia nzima.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako