Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uganda ya mchezo wa Raga, Tolbert Onyango amefanya mabadiliko katika kikosi chake na kuwaita nyota wa kimataifa wa nchi hiyo wanaocheza ligi za kulipwa nje ya nchi ili kuimarisha timu itakayoshiriki mashindano ya jumuiya ya madola.
Wachezaji hao ni Phillip Wokorach, Pius Ogena na Lawrence Sebuliba ambao sasa watachukua nafasi za Timothy Mudoola, Al Hadji Manano na James Ijongat walioondolewa.
Uganda iko katika kundi E la mashindano ya jumuiya ya madola pamoja na timu za Sri Lanka, Fiji na Wales.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |